
Hakuna mashaka yoyote unapozungumzia habari za mziki wa dansi nchini,uwezi kukosa tugusia bendi kongwe "Msondo Ngoma Band" aka baba ya mziki, wazee wa mambo hadharani.Pia utakubaliana na mimi kuwa Msondo Ngoma band ina haki ya kujigamba katika kila hali kuwa ndiye baba wa mziki,na ndio bendi pekee iliyomudu misuko suko na mawimbi ya kila aina katika gemu la mziki wa dansi! kama utakubali au la! bendi hii maarufu hapa nyumbani ndio bendi pekee kongwe ya mziki wa dansi barani Afrika,kutokana na utafiti unavyoonyesha,msondo ilizaliwa 1964 kama Nuta jazz ilikuwa inamilikiwa na umoja wa wafanyakazi(NUTA),baadae JUWATA na sasa inajitegemea,Bendi hii maarufu ina CD "Best of Msondo Ngoma" ambayo inapatikana katika maduka ya STRENE Music mjini London,Uingereza aka kwa bi.mkubwa Ukerewe,CD hiyo pia inapatikana katika maduka mbali mbali ya ughaibuni,juhudi za kuitangaza CD hiyo zimefanywa na "Ujamaa Record" ya Uingereza,kwa moyo wao wa kizalendo "Ujamaa Record" wamefanya kitendo ambacho washabiki na wapenzi wa dansi la bongo,wanaweza kuinunua CD hiyo na kujivunia kuwa Tanzania ina "baba ya mziki", ambayo tena ni bendi kongwe kuliko zote barani Afrika! kongwe kwa sababu bendi zote zilizozaliwa umri sawa na "Msondo Ngoma" kwenye miaka ya 60s hazipo tena, yaani marehemu!zimekufa,tulikuwa tunasema kuwa bendi kongwe ni TPOK Jazz iliyoanzishwa mwaka 1956 ya marehem Franko Rwambo Makiadi,nayo alipokufa Franko,bendi ikajibadili jina kutoka OK na kuitwa Bana OK! ndio kimoja.ilijikongoja lakini wapi?bendi kongwe ingine kule Kinshasa ni "Zaiko langa langa" lakini Msondo Ngoma bado kongwe kwani ina umri mrefu kuliko zaiko,na kama tukienda kule Senegar kuna watu wazima wa bendi ya Baobab Band lakini bendi hiyo ilianzishwa miaka 1970s,Msondo Ngoma bado babu yao! hata bendi maarufu ya mziki wa Salsa, AFRICANDO ambayo inawanamziki mchanganyiko kutoka karebian na Afrika magharibi,haiwezi kufikia umri wa Msondo Ngoma band babu yao!
kwani bendi ya Africando ilianzishwa miaka ya 1970 na kina marehemu Peppy Seck wa Senegar,wakiwamo akina Bonkana Maiga.Lakini sasa umri sio hoja bali matunda yepi tunavuna au tumeyavuna ?hili ndilo swali linalotakiwa kujiuliza,mbona wenzetu wanamejitangaza kwa wingi nje ya nchi na kuvuna walichokivuna! na kila mwaka wanapiga Tour za kimataifa! sisi tumekosea mahala gani?tufanye nini ? hili nasi tuwe kama wenzetu? Labda wadau na watanzania wenzetu mlio nje ya nchi je ! labda tungewaomba tufanye "Harambe la pamoja" hili tuzitoe nje bendi zetu nasi tuwe kama wenzetu,ndio tuseme hili haliwekani au? Najua penye nia pana njia wwe na mimi,sisi na nyinyi tunaweza kuufanya huu mziki wa Tanzania ukawa wa kimataifa,bendi zetu zinahitaji msaada na mchango wenu,promotion na kadhalika na hayo yote hayawezi kufanywa na wana mziki bali mimi na wewe,au sisi na wewe.
Ni mimi Malikia wako Sophia Kessy katika kukuza na kuendeleza sanaa na mziki,usikose kunitumia barua pepe kama unaushauri kwa nyie wenzetu milio nje ya nchi na ndani pia.Nimalizie makala hii kwa wito wa vionjo vya msondo "Kidogo tu! Kidogo tu! haya twendeee!!!!!